Waziri Mchengerwa aielekeza TPSC kutoa mafunzo yatakayoimarisha uzalendo kwa watumishi, Watanzania

Na James K. Mwanamyoto, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa maelekezo kwa Uongozi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) kutoa mafunzo yatakayoimarisha Uzalendo na Utaifa ili kuzalisha Watumishi wa Umma na Watanzania wazalendo watakaoshiriki vema katika kujenga uchumi wa taifa.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akiongoza maandamano wakati mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na wahitimu wakati wa mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wahitimu wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa alipokuwa akizungumza nao wakati wa mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika mahafali ya 33 ya chuo hicho yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, Mhe. Mchengerwa amesema kutokana na changamoto ya uzalendo kwa baadhi ya Watanzania, ni muda muafaka sasa kwa kila mtanzania kuwa mzalendo kwa taifa lake kwa lengo la kulinda rasilimali za taifa hivyo ni vema chuo kikajikita pia katika mafunzo ya uzalendo na utaifa.

Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa wahitimu wakiwa na uzalendo watatumia vema mafunzo waliyoyapata ili kuleta tija hususan katika kukuza uchumi wa taifa letu.

“Mafunzo mliyoyapata yasiishie hapa bali yawe ni nyenzo na mkawe mabalozi wazuri kwa kutekeleza majukumu yenu kwa weledi mkubwa na uadilifu,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Florence Turuka akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa kuzungumza na wahitimu wakati wa mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC), Dkt. Selemani Shindika akielezea lengo la kuanzishwa kwa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wakati wa mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Katika kuwajengea uwezo Watumishi wa Umma, Mhe. Mchengerwa ametoa rai kwa Viongozi wa taasisi za Umma na Halmashauri mbalimbali nchini kutenga bajeti itakayowawezesha watumishi wao kushiriki mafunzo katika chuo cha utumishi wa umma yatakayowajengea uwezo kiutendaji.

Mhe. Mchengerwa ameongeza kuwa, kuwajengea uwezo Watumishi wa Umma ni mojawapo ya utekelezaji wa Ilani cha Chama cha Mapinduzi ya 2020, hivyo ameiagiza Bodi ya Ushauri na Uongozi wa Chuo kufanya mawasiliano kwa lengo la kuzihimiza wizara na taasisi zote za serikali ili watumishi wanaostahili kupata mafunzo katika Chuo cha Utumishi wapate fursa hiyo.

“Pamoja na utekelezaji wa Ilani ya CCM, dunia inabadilika kutokana na kukua kwa teknolojia, hivyo ni lazima watumishi washiriki mafunzo mara kwa mara kuendana na mabadiliko hayo.” Mhe. Mchengerwa amesema.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa akitunuku cheti kwa mmoja wa wahitimu kwenye mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Wahitimu na wageni waalikwa wakiwa kwenye mahafali ya 33 ya chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) yaliyofanyika leo katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Sanjari na hayo, Mhe. Mchengerwa ameupongeza uongozi wa chuo na Wakufunzi kwa kutekeleza majukumu yao ya msingi ya chuo na kuaigiza Bodi na uongozi kutekeleza maelekezo ya viongozi mbalimbali ya kusogeza huduma kwa wananchi kwa kuanzisha matawi mengi zaidi ya chuo na kubuni mikakati mbalimbali itakayosaidia chuo hiki kuwa chuo cha mfano ndani na nje ya nchi.

Akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Waziri Mchengerwa kuzungumza na wahitimu, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Florence Turuka amesema wahitimu wamepata mafunzo mazuri yenye weledi mkubwa na kuwasihi wahitimu hao kutumia ujuzi na maarifa waliyoyapata kwa maslahi mapana ya taifa.

“Kutokana na mafunzo mliyoyapata hapa naamini mtakuwa ni chachu ya maendeleo na mabalozi wazuri wa chuo chetu huko muendako,” Dkt. Turuka amesisitiza.

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo na Mtendaji Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, Dkt. Selemani Shindika amesema chuo hicho kilianzishwa mwaka 2000 chini ya Sheria ya Wakala Na. 30 ya mwaka 1997 kupitia Mpango wa Uboreshaji Utumishi wa Umma (PSRP) kwa lengo la kubadilisha na kuboresha Utumishi wa Umma pamoja na kutoa mafunzo kuhusu Utumishi wa Umma, kuratibu na kujenga utamaduni mpya wa Watumishi na Watumishi wa Umma watarajiwa kujiendeleza ili kutoa huduma kwa weledi na ufanisi zaidi.

Dkt. Shindika amesisitiza umuhimu watumishi wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza kushiriki mafunzo elekezi katika Chuo cha Utumishi wa Umma ili kuwawezesha watumishi hao kufanya kazi kwa weledi na ufanisi.

Jumla ya wahitimu 7136 kutoka kwenye kozi 12 zinazotolewa na Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania wametunukiwa Astashahada ya Awali, Astashahada, Stashahada na Shahada katika fani mbalimbali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news