WAZIRI NCHEMBA: UPEKUZI WA WATEULE NI ENDELEVU

Na Saidina Msangi, WFM, Dodoma

Serikali imesema kuwa siyo sahihi kuwa na Kanzidata ya Upekuzi (Benki ya Waliopekuliwa) ili kurahisisha mchakato wa upekuzi kwa kuwa utendaji na mienendo ya maafisa hubadilika kuendana na wakati husika.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), alipokuwa akijibu swali bungeni kuhusu ucheleweshaji wa uteuzi wa Bodi za Taasisi, bungeni jijini Dodoma.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Ukonga alieitaka Serikali kuanzisha Benki ya waliopekuliwa kwa ajili ya uteuzi ili kurahisisha zoezi la uteuzi wa Bodi za Taasisi na kuziwezesha Taasisi hizo kwenda na kasi ya Mhe. Rais kwa kile alichosema kuwa upekuzi umekuwa kisingizio cha kuchelewesha uteuzi.

“Upekuzi kwa ajili ya kujaza nafasi mbalimbali hufanyika kwa wakati husika kutokana na ukweli kwamba utendaji na mienendo ya maafisa pia hubadilika kutoka wakati mmoja hadi mwingine,” alifafanua Mhe. Nchemba.

Aidha, alieleza kuwa Wizara ya Fedha na Mipango ina jumla ya Taasisi 28 ambazo inazisimamia, kati ya hizo, Taasisi Tisa (9) Bodi zake zimemaliza muda wake.

Mhe. Nchemba alisema kuwa mapendekezo ya majina kwa ajili ya kujaza nafasi za Wenyeviti na Wajumbe wa Bodi hizo yamewasilishwa kwenye Mamlaka za Upekuzi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news