Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kujenga kilometa 1,495.45 za barabara kwa kiwango cha lami pamoja na madaraja makubwa 18 ndani ya kipindi cha miaka mitano, hatua iliyoelezwa kuwa mafanikio makubwa katika sekta ya miundombinu nchini.
Mafanikio hayo yameelezwa Jumatano Mei 20, 2026 bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka wa fedha 2026/2027.Waziri Ulega amesema mtandao wa barabara za kitaifa unaosimamiwa na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) umefikia kilometa 37,734.41, ambapo kati ya hizo kilometa 12,225.26 zimejengwa kwa kiwango cha lami.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo















