Magazeti leo Mei 22,2026

Makatibu Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanaosimamia masuala ya mtangamano wamekutana katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya Mkutano Maalumu wa 60 wa Baraza la Mawaziri la EAC unaotarajiwa kufanyika tarehe 22 Mei 2026.
Kikao hicho cha Makatibu Wakuu kimepokea, kujadili na kupendekeza rasimu ya mapendekezo ya bajeti ya Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/2027, ambayo itawasilishwa katika Mkutano Maalumu wa Mawaziri kwa ajili ya idhini.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Stephen Patrick Mbundi, alisisitiza umuhimu wa mkutano huo, akieleza kuwa kupitishwa kwa mapendekezo hayo ya bajeti kutasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekretarieti na taasisi zake, ikiwemo uhaba wa watumishi pamoja na ulipaji wa madeni ya watoa huduma.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here