Breaking News: Waziri Aweso avunja kamati ya maji, upigaji mamilioni

Na Robert Kalokola, Diramakini Blog

Waziri wa Maji Jumaa Aweso amevunja Kamati ya Maji ya Jumuiya ya Watumia Maji ya Kijiji cha Mharamba,Kata ya Nkome wilayani Geita baada ya kubaini dalili za ubadhirifu katika makusanyo ya maji katika mradi wa Mharamba.

Waziri wa Maji Jumaa Aweso akizungumza katika mkutano wa hadhara katika Kijiji Cha Mharamba ,Kata ya Nkome Wilaya ya Geita (Robert Kalokola/DIRAMAKINI BLOG).

Mwenyekiti wa Kamati hiyo alimueleza Waziri wa Maji kuwa kamati hiyo ina laki tano benki lakini baada ya mahojiano na Waziri ikaonekana kamati ilipaswa kuwa imekusanya zaidi ya milioni 20.

Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Geita Wilson Shimo ameagiza Mkuu wa Polisi Wilaya ya Geita na Takukuru kuwakamata Mwenyekiti,Katibu na Mweka hazina wa kamati hiyo ili kufanya uchunguzi wa mapato na matumizi ya mradi huo. 
 
HABARI ZAIDI ZINAKUJIA HAPA PUNDE

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news