Jeshi la Polisi lataja majina ya Wanafunzi watatu walioliwa na simba

Na Abe Paul, Jeshi la Polisi Arusha

WANAFUNZI watatu katika Shule ya Msingi Ngoile wanaoishi Kijiji cha Ngoile wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wamefariki dunia baada ya kuliwa na simba.
Akizungumza tukio hilo leo Agosti 5,2021 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema watoto hao wameuawa Agosti 3 mwaka huu na amewataja wanafunzi hao ni Olobiko Metui(10),Ndaskoi Sangu (9) na Sanka Saning'o( 10) ambao wote ni wanafunzi wa darasa la tatu.

"Watoto hao kabla ya kuuawa alishambuliwa na Simba,"amesema.

Pia mtoto mwingine aitwaye Kiambwa Lektonyi(11) alijeruhiwa na kundi hilo la simba ambao jumla yao ni watoto wanne wote wanafunzi wa shule ya msingi Ngoile.

Kamanda Masejo amesema kuwa, chanzo cha tukio hilo ni baada ya wanafunzi hao kutoka shule ambapo walifika majumbani mwao na walikwenda kutafuta mifugo yao iliyokuwa imepotea porini kitendo kilichopelekea kushambuliwa na wanyama hao wakali aina simba.

Ameleza kuwa, majeruhi amelazwa katika Zahanati ya Kata ya OLBALBAL kwa matibabu zaidi pia miili ya marehemu wote imefanyiwa uchunguzi wa kidaktari na ndugu wa marehemu wamekabidhiwa miili hiyo.

Ametoa mwito kwa jamii za kifugaji kuchukua tahadhari kwa watoto wadogo pindi wanapowapa majukumu ya uangalizi (kuchunga) mifugo hususani katika vijiji vinavyopakana na hifadhi ili kuepusha madhara makubwa ambayo yaweza kutokea katika majukumu yao ya uangalizi wa mifugo pamoja na familia zao.

Pia niendele kuwasihi wananchi kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwa Jeshi la Polisi ili kukomesha vitendo vya kiahalifu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news