MBUNGE NEEMA LUGANGIRA ATEULIWA KUWA BALOZI WA COVID-19

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

MBUNGE wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Neema Lugangira ameteuliwa kuwa Balozi wa hamasa dhidi ya mapambano ya virusi vya Corona (COVID-19).

Mheshimiwa Neema Lugangira ameteuliwa Agosti 12,mwaka huu na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Dkt. Dorothy Gwajima mkoani Dar es Salaam.
Mbunge Neema Lugangira ambaye pia ni Balozi wa Covid-19 akiwa na bango la kuhamasisha uvaaji wa barakoa na wananchi kuhakikisha wanachanja na kuzingatia miongozo mingine ya Afya.

Mbali na Mbunge Neema Lugangira wengine walioteuliwa ni msanii maarufu nchini na Mwenyekiti wa Jukwaa la Mama Ongea na Mwanao, Steven Mengele 'Steve Nyerere' na Mwanaharakati wa Kutetea Haki za Wanawake nchini, Joyce Kiria.
Mbunge wa Neema Lugangira ambaye pia ni Balozi wa Covid-19 wa kwanza kulia akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Afya Maendeleo Jinsia Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima. Akifuatiwa na Msanii maarufu nchini na Mwenyekiti wa Jukwaa la Mama Ongea na Mwanao, Steven Mengele 'Steve Nyerere' na Mwanaharakati wa Kutetea Haki za Wanawake nchini, Joyce Kiria.
Hatua hii inakuja ikiwa tangu janga la Corona liingie nchini kwenye Wimbi la Kwanza hadi sasa Wimbi la Tatu, Mbunge Neema Lugangira ameonyesha jitihada mbalimbali za kupambana na janga hilo.

Miongoni mwa jitihada hizo ni pamoja na kuelimisha, kutoa mahitaji ya kukabiiana na maambukizi na kuhamasisha Watanzania kujikinga na kuchanja ili kujikinga dhidi ya ugonjwa huo hatari ambao umeathiri maeneo mengi duniani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news