Magazeti leo Julai 21,2026

Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu ametaka watumishi wa umma wote wanaodaiwa kuhusika na ubadhirifu wa fedha za mradi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Msingi Mfinga kufikishwa mahakamani haraka baada ya kubainika kuwepo kwa viashiria vya matumizi mabaya ya fedha za umma.Akizungumza Julai 19,2026 baada ya kukagua mradi huo wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya kuhamasisha shughuli za maendeleo katika Jimbo la Kwela, na kueleza kuwa hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo licha ya fedha nyingi zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wake.
Ameeleza kuwa kati ya shilingi milioni 220.1 zilizotolewa kwa mradi huo tangu Julai 2025, tayari shilingi milioni 212.9 zimetumika lakini ujenzi bado haujakamilika jambo ambalo linaibua maswali kuhusu uwajibikaji na usimamizi wa fedha za umma.







Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here