MWILI WA ALIYEKUWA WAZIRI WA ULINZI ULIVYOWASILI NYUMBANI KWAKE


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akiongoza mamia ya waombolezaji waliofika katika msiba wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, John Elias Kwandikwa kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu mkoani Shinyanga.
Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa uikisindikizwa na Makamanda wa JWTZ kutoka kwenye nyumba yake kuelekea eneo maalum kwa ajili ya kutoa nafasi kwa wana Ushetu kuaga mwili huo kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga.
Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa uikisindikizwa na Makamanda wa JWTZ kutoka kwenye gari maalum la kijeshi ili kupelekwa nyumbani kwake kabla ya kuendelea na taratibu za kuaga mwili huo kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga.
Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa ukiwa umewasili kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga kwa ajili ya wananchi wa wake kuanza kujiweka tayari kuanza taratibu za kuaga na baadaye kesho kuwekwa katika nyumba yake ya milele.
Makamanda wa Jeshi la JWTZ wakitoa heshima kwa viongozi mbalimbali waliofika nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Ulinzi Marehemu John Elias Kwandikwa kwa ajili ya kuanza taratibu za kuaga na baadaye kesho kupumzisha mwili huo katika Nyumba yake ya milele kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga.(Picha zote na Anthony Ishengoma).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news