James Rugemalira aachiwa huru

KISUTU, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia mashtaka na kumwachia huru mfanyabiashara maarufu Tanzania, James Rugemalira.

Hatua hiyo inatokana na Mkurugenzi wa Mashataka nchini (DPP) kueleza kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo dhidi ya mshtakiwa huyo.
Akizungumza muda mfupi baada ya kuachiwa leo Septemba 16, 2021, Mike Ngalo ambae ni wanasheria wa Rugemalira amesema mteja wake amefutiwa mashtaka yote baada ya DPP kusema kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo.
 
Juni 2017, Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini Tanzania (TAKUKURU ) iliwafikisha Mahakamani Mkurugenzi wa Kampuni ya Kufua Umeme (IPTL), Herbinder Seth na Rugemalira kwa makosa sita ya uhujumu uchumi ikiwemo kosa la kuisababishia serikali hasara.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news