Simiyu yashika nafasi ya nne kutoka 20 Kitaifa miradi ya Mwenge wa Uhuru

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Mkuu wa Mkoa Simiyu, David Kafulila Novemba 11,2021 amewapongeza wakurugenzi na wakuu wa wilaya tano za Mkoa wa Simiyu kwa kuendelea kuboresha usimamizi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Amesema ni juhudi hizo zilizofanikisha Mkoa wa Simiyu kushika nafasi ya nne mwaka huu 2021 kutoka nafasi ya 20 mwaka 2020.
"Mimi naona fahari kuwa na timu hii ya wakuu wa wilaya na wakurugenzi. Mbali ya kupaisha mkoa huu kutoka nafasi ya pili mkiani mwaka 2020 mpaka nafasi ya pili juu katika makusanyo ya halmashauri kimkoa, leo nimepata taarifa kuwa mkoa wetu umeshika nafasi ya nne kitaifa katika miradi ya Mwenge iliyokaguliwa kulinganisha na nafasi ya 20 mwaka 2020.

"Ninaamini mwakani tutashika nafasi ya kwanza.Angalia hapa Busega, taarifa ya makusanyo ya robo ya mwaka wa fedha 2020 ilikuwa asilimia 15 ya lengo kulinganisha na asilimia 29 kwenye robo ya kwanza mwaka 2021. Hivyo inawezekana. Tuendelee kupambana kujenga mkoa wetu," alisisitiza Kafulila katika hotuba yake kwenye Baraza la Madiwani wilaya ya Busega.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news