Shughuli za binadamu zatajwa kuwa kikwazo Mto Zigi

NA HADIJA BAGASHA

JITIHADA za haraka zimetakiwa kufanyika ili kukabiliana na shughuli za kilimo na uchimbaji wa madini unaofanywa kwenye vyanzo vya maji vya Mto Zigi ambao ni tegmeo la wakazi wa jiji la Tanga na maeneo mengine ya mkoa wa Tanga.
Hayo yamesemwa wakati wa kikao cha pili cha Jukwaa la Wadau wa Kidakio cha Mto Zigi waliokutana jijini Tanga kujadili changamoto zinavyovikabili vyanzo vya maji na kuangalia namna ya kuvinusuru dhidi ya shughuli za kibinadamu.

Wadau wa jukwaa hilo wamezungumzia uharibifu wa vyanzo vya maji vya Mto Zigi, uharibifu unaotokana na shughuli za kibinadamu ikiwemo uchimbaji wa madini.
Wadau hao akiwemo Amiri Mduruma ambaye ni Mkurugenzi Aminata Guality SEED na Philip Mdoe Mwenyekiti Jumuiya za watumiaji wa maji Zigi Juu wamesema jambo hilo bado ni tatizo hivyo ni vyema wakashirikiana na wizara ili kunusuru vyanzo hivyo.

Abrahamu Isaya ni kaimu mkurugenzi bodi ya maji Bonde la Mto Pangani amesema kwamba, changamoto walizokuwa nazo katika usimamizi wa rasilimali za maji kuwa bado ni kubwa ukilinganisha na mafanikio ambayo wameyapata.
“Kiukweli tumefanikiwa katika eneo kubwa lakini tunaendelea kuongeza jitihada ndio maana leo hii tumekaa kikao kazi cha pili kwajili ya kuhakikisha kwamba lengo la serikali la kusimamia rasilimali za maji zinakuwa endelevu,”alisisitiza Issaya.

Naye Rosemery Rwebugisa ni kaimu Mkurugenzi Wizara ya Maji, idara ya Rasilimali Maji amesema kwamba hivi karibuni wameona kuna changamoto ya uharibifu wa vyanzo vya maji kutokana na uvamizi wa jamii kwajili ya kufanya shughuli za kimaendeleo ikiwemo kilimo,mifugo,na hata ufyatuaji wa matofali sambamba na kumwaga maji taka kwenye vyanzo hivyo.
Mkuu wa wilaya ya Tanga,Hashim Mgandilwa katika kikao hicho ametoa rai kwa jumuiya za watumiaji wa maji na kuwataka pindi wanapokusanya fedha za jumuiya kuacha kuzitumia katika matumizi ambayo si sahihi.

“Hizi jumuiya zinapoanza kukusanya fedha na zikawa na fedha kwao inakuwa ni mtihani leo tumekaa wenyewe, lakini mkipata fursa siku moja tokeni nendeni mkakae na hizo jumuiya kwenye mikutano yao mtajifunza kitu moja ya kitu ambacho kipo wanakusanya fedha nyingi mwisho wa siku fedha hizi wanazitumia ovyo,”amesisitiza DC Mgandilwa.

Mto Zigi ndio mto pekee unaotegemewa na wakazi wa Wilaya ya Tanga na kwamba kama shughhuli za kibinadamu zitaendelea kushamiri kwenye mto huo upo uwezekano wa jiji la Tanga kuingia kwenye shida ya maji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news