Faru Rajabu afariki, TANAPA yathibitisha

*Alikuwa na umri wa miaka 43

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) limethibitisha kuwa, Faru Rajabu amefariki usiku wa kuamkia leo Machi 21,2022 akiwa na umri wa miaka 43.
Faru Rajabu alikuwa mtoto wa faru maarufu aliyejulikana kama Faru John aliyefariki mapema mwaka 2015 akiwa na umri wa miaka 47.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Pascal Shelutete inaeleza kuwa Faru Rajabu alifariki katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na sababu ya kifo chake ikitajwa kuwa ni uzee.
“Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) linasikitika kutangaza kifo cha Faru Rajabu mwenye umri wa miaka 43 kilichotokea usiku wa kuamkia leo kutokana na sababu ya uzee katika Hifadhi ya Taifa Serengeti,” imeeleza sehemu ya taarifa ya TANAPA.

Kwa mujibu wa TANAPA mwili wa faru huyo utahifadhiwa kwa mujibu wa kanuni za asili za uhifadhi.

Faru Rajabu ambaye alizaliwa kwenye eneo Ngorongoro mwaka 1979 na mwaka 1993 alihamia katika Hifadhi ya Serengeti ameacha watoto, wajukuu na vitukuu kadhaa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news