Utabiri wa hali ya hewa Tanzania saa 24 zijazo...Next 24 hours Weather forecast

UTABIRI wa hali ya hewa saa 24 zijazo kuanzia leo saa tatu usiku Machi 13, 2022 unawasilishwa na mchambuzi, Bi.Tabu Kwedilima kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA).
Kwa mujibu wa TMA, mikoa ya Ruvuma, Morogoro (Kusini), Kigoma, Katavi, Tabora, Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe, Kagera, Geita, Mwanza, Mara, Shinyanga na Simiyu kuna matarajio ya mvua,ngurumo na jua katika maeneo machache.

Aidha, mikoa ya Lindi, Mtwara, Dodoma na Singida kuna matarajio ya mvua nyepesi na jua katika maeneo machache.

Kwa upande wa Visiwa vya Unguja na Pemba, Dar es Salaam, Tanga, Morogoro (Kaskazini), Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia kuna matarajio ya jua.

UPEPO WA PWANI

Kwa mujibu wa TMA, upepo huo unatarajiwa kuvuma kutoka Mashariki kwa kasi ya kilomita 30 kwa saa kwa Pwani ya Kaskazini na kutoka Kaskazini Mashariki kwa kasi ya kilomita 20 kwa saa kwa Pwani ya Kusini.

HALI YA BAHARI

Mawimbi madogo hadi makubwa kiasi yanatarajiwa katika bahari.


TANZANIA WEATHER FORECAST 13/03/2022

THUNDERSHOWERS ARE EXPECTED OVER MWANZA, SHINYANGA, SIMIYU, MARA, GEITA, KAGERA, TABORA, KIGOMA, KATAVI, RUKWA, MBEYA, SONGWE, MOROGORO(KUSINI), IRINGA, NJOMBE AND RUVUMA REGIONS.

Weather forecast for this weekend, as presented by Ramadhani Omary from Tanzania Meteorological Authority (TMA).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news