Jeshi la Uhamiaji ladaka Wahabeshi jijini Dodoma

NA DOREEN ALOYCE

JESHI la Uhamiaji Mkoa wa Dodoma linawashikilia raia watano wa Ethiopia akiwemo Mtanzania mmoja kutokana na kuingia nchini kinyume cha sheria na utaratibu wa nchi.
Pia linamshikilia raia mmoja wa Tanzania, Tito Mbwilo mwenye umri wa miaka 43 mkazi wa Iringa na Tunduma ambaye alikuwa akisafirisha wahamiaji hao.
Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dodoma, Bahati Mwaifuge ameyasema hayo wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ambapo alisema kuwa wahamiaji hao haramu walikamatwa Aprili 3, mwaka huu katika Kijiji cha Mtera wakielekea Tunduma Mkoa wa Songwe.

"Jeshi letu la uhamiaji tumefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu watano akiwemo mtanzania mmoja wakisafirishwa kwenye gari yenye namba za usajili T991 DXB Toyota Rumion ambalo lilikuwa linaendeshwa na Tito Mbwilo akijua ni kosa,"alisema Bahati.
Aidha, alisema baada ya kuwatia mbaroni wahamiaji haramu hao, dereva wao Tito Mbwilo alijaribu kutoroka bila mafanikio kutokana na umahiri wa askari ambapo waliweza kimdhibiti na kumuweka chini ya ulinzi.

Hata hivyo, alitoa onyo kwa wasafirishaji wote wanaojihusisha na wahamiaji haramu katika Mkoa wa Dodoma kuacha mara moja na kwamba jeshi tayari limebaini wamebadili mbinu kutoka magari makubwa na kutumia magari madogo.

"Niwaombe wananchi wote wakiwemo wa Mtera kuendelea na ushirikiano kutoa taarifa za kusafirisha wahamiaji haramu jambo ambalo litasaidia katika utendaji kazi wetu,"alisema Bahati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news