Rais Samia aridhia nyongeza ya mishahara kwa asilimia 23.3

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ameridhia mapendekezo ya kuongeza mishahara ikiwemo kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa asilimia 23.3, ambapo shilingi trilioni 1.59 itatumika kwa ongezeko hilo.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Mei 14, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus.

Taarifa hiyo inasema, mapendekezo hayo ni mwendelezo wa kikao cha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alichokifanya hivi karibuni mkoani Dodoma na kupokea taarifa kutoka kwa wataalamu kuhusu ongezeko la mishahara.

Pia taarifa hiyo imesema Serikali imepanga kutumia kiasi cha shilingi trilioni 9.7 katika mwaka wa fedha 2022/23 kwa ajili ya kugharamia malipo ya mishara ya watumishi wote katika Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi na Wakala za Serikali.

“Bajeti ya mishahara ya mwaka 2022/23 inaongezeko la shilingi trilioni 1.59 sawa na asilimia 19.51 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka wa fedha wa 2021/22,” imefafanua taarifa hiyo.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

1 Comments

  1. Sekta binafsi ni watumishi lakini kwa serikali ya jamuhuri ya mungano wa Tanzania awatambuliki .ata mama yetu ameshindwa kuwaongelea ongezeko la mishaara mipya.

    ReplyDelete
Previous Post Next Post

International news