SERIKALI YAENDELEA KUHIMIZA WANACHI UWEKAJI ANWANI ZA MAKAZI

NA MWANDISHI WETU

NAIBU Katibu Mkuu, Bw. Kaspar Mmuya amehimiza wananchi ambao bado maeneo yao hayajatambuliwa kwenye zoezi uwekaji anwani za makazi kujitokeza kwenye Ofisi za serikali za Mitaa au Kijiji kueleza ili uongozi uwawekee namba.
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Bw. Kaspar Mmuya akizungumza katika ziara yake ya kukagua zoezi la uwekaji wa anwani za makazi Mkoani Lindi alipotembelea Halmashauri ya Mtama na Manispaa ya Lindi.

Amesema hayo katika ziara yake ya kikazi Mkoa wa Lindi alipotembelea kujionea utekelezaji wa zoezi la anwani na makazi ambalo limeweza kutambua barabara na mitaa 7972 na majengo na viwanja 334771 vimeweza kutambuliwa na kuingizwa kwenye mfumo wa NAPA.

“Mkoa wa Lindi umefaulu vizuri sana katika kuweka miundo mbinu hasa ya barabara na wamefanikiwa vizuri kuyatambua maeneo yake na kuyapa namba ikiwa inamaanisha nyumba na barabara nyingi kutambuliwa kwa majina alisema Naibu Katibu Mkuu,"amesema.
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Bw. Kaspar Mmuya akiangalia Ubunifu wa kupaka rangi na kuandika postikodi kwenye nyumba katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa zoezi la uwekaji wa anwani za makazi katika Mkoa wa Lindi.

Ameongeza kuwa, mitaa ambayo haijabandikwa kibao na jina nimepewa mpango kazi na miundo mbinu inatengenezwa kwa kushirikiana vizuri na TANROAD pamoja TARURA katika barabara zinazohusu taasisi zetu hizi mbili.

"Uelewa wa wananchi katika kulipokea na kulitekeleza jambo hili ni mkubwa kwa sababu wameshirikishwa katika kutafuta majina hayo ya mitaa na wanajua umuhimu wa kuwepo kwa miundo mbinu hiyo,"amesema.
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Bw. Kaspar Mmuya akishiriki kuweka kibao cha postikodi katika Halmashauri ya Mtama Kijiji cha Masasi Mtaa wa Mama Samia katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa zoezi la uwekaji wa anwani za makazi katika Mkoa wa Lindi.

“Wananchi walio wengi wamekubali kuzichora nyumba zao kwa kutumia rangi ya njano na kuweka namba katika nyumba kwa kutumia rangi nyeusi, ni wajibu wetu kama kanuni za anwani za makazi ambazo zimewekwa na TAMISEMI kanuni namba 20 ambayo inasema ni wajibu wa mwenye nyumba kuweka namba hiyo kwenye nyumba yake," amesema Naibu Katibu Mkuu.
Naibu katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu, Bw. Kaspar Mmuya akishiriki kuweka kibao cha postikodi katika Manispaa ya Lindi kata ya Konde katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa zoezi la uwekaji wa anwani za makazi katika Mkoa wa Lindi.

Akihitimisha Kaimu Meneja wa TARURA Mkoa wa Lindi, Mhandisi Dawson Paschal amesema watawekwa nguzo na vibao 3042 katika Mkoa mzima wa Lindi. Vibao vitakavyotengenezwa vitafidia sehemu ambazo hazijawekwa ili kuhakikisha zoezi la uwekaji wa miundo mbinu linafanikiw.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news