DC James:Viongozi wa dini tumieni nafasi zenu kutoa elimu ya Sensa

NA DIRAMAKINI

MKUU wa Wilaya ya Ubungo, Heri James amewataka viongozi wa dini nchini kutumia nafasi zao kutoa elimu juu ya umuhimu wa sensa, kwani kufanya hivyo kunatoa fursa kwa Serikali kuwafikia wananchi wake kimaendeleo.
Mkuu wa Wilaya ya Ubongo Kheri James (kulia) akikabidhi makusanyo kwa Mwenyekiti wa Chama kipya cha Umoja wa Wababa Kanisa la Anglicana Achidikonari ya Ubungo (UBAKI) Moses Manyatta (kushoto) yaliyokusanywa kutoka kwa washarika na waumini wa kanisa hilo (hawamo pichani) wakati wa sherehe za kuzindua rasmi Umoja huo zilizofanyika leo Juni 11,2022 katika kanisa la Mtakatifu Batolomayo Ubungo Jijini Dar es Salaam.

Amesema, mwaka huu Agosti 23 ni mwaka wa sensa hivyo ni vema viongozi wakahamasisha wananchi wao na kuwakumbusha umuhimu wa kuhesabiwa ukizingatia zoezi hilo linafanyika kila baada ya miaka kumi.
Mkuu wa Wilaya ya Ubongo Kheri James akizungumza alipokuwa akitoa hotuba yake katika hafla hiyo muda mfupi baada ya kuzindua rasimi Umoja wa Chama cha Wababa (UBAKI) wa Kanisa Anglicana katika Wilaya ya Ubungo.

DC James ametoa kauli hiyo leo Juni 11, 2022 mkoani Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa umoja wa Chama cha Wababa (UBAK) wa Kanisa la Angalikana Archidikonary ya Ubungo uliofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Barthromayo wilayani humo.
"Kwanza nawapongeza kwa uzinduzi huu wa Chama cha wababa kwani kimekuja wakati sahihi ukizingatia mara zote tumekuwa na mambo ya akina mama tu hivyo Chama hiki ni sehemu ya juu kwa wababa katika kuwasilisha na kutoa maoni yao. Lakini pia tutumia umoja huu kukumbushana juu ya kulinda maadili yetu na malezi kwa vijana wetu,"amesema.
Kwaya ya Umoja wa Wakina Baba kutoka katika Kanisa la KKKT Usharika wa Makongo Juu wakitumbuiza kwenye hafla hiyo.
Wanachama wa UBAKI na wageni mbalimbali waalikwa wakiwa kwenye maandamano maalum yaliyoanza mapema Asubuhi ya leo Juni 11,2022 kutokea Shekilango hadi kwenye kanisa hilo kwaajili ya Ibada fupi iliyofanyika Kanisani hapo kabla ya kuanza shamrashamra za uzinduzi rasmi wa Umoja huo.  

"Serikali hususani Wilaya yangu ya Ubungo tuna mashirikiano mazuri na Kanisa la Anglikana kupitia viongozi wake, ni matumaini yangu hata katika hili la UBAKI tutaendelea kushirikiana pasipo shaka.
Pia amewahamisha waumini hao kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo wilayani humo hususani mikopo ambayo inatolewa bila riba kupitia halmashauri ya Ubungo,nakwamba wilaya hiyo ndio lango kuu la kuingilia mjini kati na hata stendi ya Magufuli ipo ubungo hivyo ni muhimu kuwa na jicho la kutazama fursa zilizopo za kiuchumi.

"Ndungu zangu kupitia Umoja huu tuimarishe malezi kwa vijana ,maadili ,na tuendelee kukemea wizi,ufisadi,dhuluma,ukatili na uhujumu kwani haya yote ni roho zisizokubarika katika jamii yetu"amesisitiza James.
Mwnyekiti wa UBAKI Mosses Manyatta akizungumza akelezea majukumu ya chama hicho mapema mara baada ya kuwasili mgeni rasmi kwenye hafla hiyo iliyofanyika leo Juni 11,2022 jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Kasisi Kiongozi wa Kanisa la Angalikana Dayosisi ya Dar es Salaam, Richard Kamenya pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha UBAKI, Moses Manyatta wamesema pamoja na mambo mengine yote lakinin pia watatumia umoja huo kuhamsisha waumini kushiriki kikamilifu katika zoezi la sensa linalotarajia kufanyika kitaifa Agosti 23 mwaka huu.
Viongozi wa UBAKI wakitambulishwa rasmi na kuwekwa wakfu kukiongoza chama hicho katika hafla hiyo. Pia wameipongeza na kuishukuru Serikali kwa ushirikiano mkubwa wanaoendelea kuutoa kwenye Taasisi za dini hivyo wao kama viongozi jukumu lao kubwa ni kuendelea kusimamia utulivu uliopo.
Wageni mbalimbali, wahumini na washarika wa kanisa hilo wakifuatilia hotuba za viongozi zilizokuwa zikitolewa kwenye hafla hiyo. (PICHA ZOTE NA HUGHES DUGILO). 

Katika uzinduzi huo wa Chama cha Umoja wa Baba (UBAKI), Mkuu wa Wilaya hiyo ya Ubungo, Heri James amechangia shilingi laki tano (500,000) kwa ajili ya kutunisha ufuko wa umoja huo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news