Rais Samia arejesha tabasamu kwa kijana mwenye ulemavu wa ngozi

NA DIRAMAKINI

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi ya kumpatia mtaji wa biashara na fedha za kujikimu shilingi milioni 5,310,000, Bw.Yassin Said mwenye ulemavu wa ngozi aliemuandikia barua Rais akiomba kuwezeshwa kiuchumi baada ya kupitia masaibu katika maisha yake.
Akikabidhi fedha hizo kwa niaba ya Rais Samia, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amemsisitiza kijana Yassin kutumia fedha alizopatiwa kujiimarisha kiuchumi ili lengo la Rais kutoa fedha hizo liweze kutimia.
Kwa upande wake, Yassin Said amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa msaada aliopatiwa na kuahidi kuzitumia kwa lengo lililokusudiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news