MFUKO wa SELF Microfinance Fund umetumia Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma kuhamasisha wananchi, wajasiriamali, wakulima na wafugaji kunufaika na huduma zake za mikopo na elimu ya fedha, hatua inayolenga kuongeza ushiriki wao katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya uchumi.


Hayo yamesemwa Juni 18, 2026 na Meneja wa Mfuko wa SELF Kanda ya Kati, Aristid Tesha, katika Viwanja vya Chinangali jijini Dodoma, ambapo taasisi hiyo inaendelea kutoa elimu na huduma mbalimbali kwa wananchi wanaotembelea banda lake.
Tesha amesema kanda hiyo inahudumia mikoa ya Dodoma na Singida na kwamba ushiriki wa SELF katika maonesho hayo unalenga kuwafikisha wananchi karibu na huduma zake pamoja na kuwawezesha kufahamu fursa zilizopo kwa ajili ya kukuza shughuli zao za kiuchumi.
Amesema tangu kuanza kwa maonesho hayo Juni 16, wananchi wengi wamejitokeza kutembelea banda la SELF kwa lengo la kupata elimu ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha na taarifa kuhusu huduma mbalimbali za mikopo zinazotolewa na mfuko huo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo







