Wahasibu, wakaguzi zingatieni Dira ya Mahakama asema Jaji Mdemu

NA INNOCENT KANSHA-Mahakama

JAJI Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu ametoa wito kwa Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani kutumia mafunzo watakayopata kuhakikisha yanatekeleza dira ya Mahakama na kusaidia kutatua kero za wadaawa ili huduma zitolewe kwa haraka, weledi, wepesi na ufanisi wa hali ya juu.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani wa Mahakama ya Tanzania wakimsikiliza Mwezeshaji (hayupo katika picha) katika Ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki jijini Dodoma.

Akifungua mafunzo ya kundi la pili la Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani ya siku tano katika Ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki jijini Dodoma tarehe 6 Juni, 2022, Jaji Mdemu alisema dira ya Mahakama haiwezi kutekelezeka iwapo mifumo ya kihasibu watakayojifunza haitosaidia kuondoa usumbufu kwa wadaawa wakati wa kufanya malipo mbalimbali ya usajili wa mashauri na nyaraka za kimahakama, kulipa mirathi kwa wakati na watumishi wa ndani kupata stahiki zao bila usumbufu na kucheleweshwa.

“Pengine jambo la msingi ambalo mnatakiwa kulifahamu na kupitia mafunzo haya mtalifahamu ni kuwa dira ya upatikanaji wa haki kwa wakati na kwa wote haitafanikiwa kwa dhana kwamba inawahusu maafisa wa Mahakama tu, bali hata ninyi pia mna nafasi kubwa ya kuhakikisha matamanio ya taasisi yanafikiwa katika utoaji wa huduma ya haki unaomlenga mteja na hivyo mtakwenda kutenda kwa vitendo”, aliongeza Jaji Mdemu.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Gerson Mdemu akisisitiza jambo wakati wa kufungua mafunzo ya Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani kundi la pili yanayofanyika kwa siku tano katika Ukumbu wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Jijini Dodoma jana kuanzia tarehe 6 Juni 2022. wengine ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Bernard Mpepo (wa kwanza kulia) na Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu (wa kwanza kushoto).

Mhe. Mdemu akatoa rai kwa Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani kutumia ujuzi na taarifa za msingi watakazobadilisha kupitia wakufunzi katika mafunzo hayo kuhusu matumizi bora ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kutatua changamoto za utoaji wa huduma za kihasibu ili kurahisisha na kuondoa usumbufu kwa wadaawa watakao wahudumia.

Alisema kuwa TEHAMA ndiyo msingi wa dira ya kurahisisha upatikanaji wa huduma, kwa kuwa washiriki hao wa mafunzo ndiyo watakaofunzwa kuhusu matumizi ya hiyo mifumo, hivyo wanapaswa kutokuwa kikwazo cha utoaji huduma bora kwa wadaawa.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo Mchumi kutoka Idara ya Mipango na Ufuatiliaji ya Mahakama ya Tanzania, Bw. Kisingi Mhando akitoa mada ya Mpango Mkakati wa Mahakama ya Tanzania Awamu ya Pili kwa washiriki hao.

“Mahakama ya Tanzania inanuwia kuwa na maamuzi bora ya kimahakama ambapo imejiwekea malengo ya kukuza uelewa wa misingi ya taaluma ya kisheria na kuongeza ujuzi kwa watumishi wa Mahakama. Katika kutekeleza malengo hayo, Mahakama imejiwekea mkakati wa kuwajengea uwezo watumishi wa ngazi zote. Mmejengewa uwezo kwenye eneo lenu la kihasibu. Sasa hakutakuwa na kisingizio cha kuchelewesha huduma, hususani masuala ya mirathi ambayo yanahitimisha maamuzi yanayotolewa na Mahakimu na Majaji”, aliongeza Jaji Mfawidhi

Jaji Mdemu akasema ratiba ya mafunzo yatahusu maeneo ambayo yameainishwa kama vile Mpango Mkakati wa Mahakama (Judiciary Strategic Plan), Njia sahihi ya kushughulikia mfumo wa masurufu (Appropriate Configuration of System Imprest Management), Jinsi ya kulipa malipo ya kabla kwenye mfumo pamoja na mzunguko wake (Recording of System Ledgers for Prepayment Transactions, Suspense Accounts and Clearing Accounts), Jinsi gani akaunti za kuhamisha fedha zinavyofanya kazi (Overview of GePG Payment Systems; Proper MUSE functions), Jinsi gani mfumo wa kielektroniki wa mapato serikalini unatoa huduma (Roles and Responsibilities of Accounts in Accounting Electronics and Technological systems),

Maeneo mengine ya mafunzo hayo yatahusu Jinsi gani mfumo wa malipo serikalini unavyofanya kazi (Ageing analysis for Debtors and Creditors in Accounting Systems; Previewing of Accounts (ledger Accounts), Mkataba wa huduma kwa mteja (Client Service Charter), Huduma kwa mteja na maadili (Customer Service and Ethics Issues) Professionalism in Accounts and Code of good conduct, Introduction to various GePG reports and their uses, Periodic GePG Reconciliation; Psychological Issues.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani wa Mahakama ya Tanzania wakimsikiliza Mwezeshaji (hayupo katika picha) katika Ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Jijini Dodoma.
Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani wa Mahakama ya Tanzania wakimsikiliza Mwezeshaji (hayupo katika picha) katika Ukumbi wa Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Jijini Dodoma.
Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu (aliyenyoosha mkono mbele) akitoa ufafanuzi wa jambo wakati wa mafunzo hayo.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo wa kada ya Wahasibu, wengine ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Bernard Mpepo (wa pili kulia) na kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma Bw. Sumera Manoti (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu (wa pili kushoto) na Muhasibu Mwandamizi Mwandamizi Mahakama ya Tanzania Bw. Venant Kambuga (wa kwanza kulia).
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo wa kada ya Wakaguzi wa Ndani, wengine ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Bernard Mpepo (wa pili kulia) na kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma Bw. Sumera Manoti (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu (wa pili kushoto) na Muhasibu Mwandamizi Mwandamizi Mahakama ya Tanzania Bw. Venant Kambuga (wa kwanza kulia).
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma, Mhe. Gerson Mdemu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Sekretarieti ya mafunzo, wengine ni Naibu Msajili Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma Mhe. Bernard Mpepo (wa pili kulia) na kushoto ni Mtendaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Dodoma Bw. Sumera Manoti (wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Msaidizi wa Mafunzo Mahakama ya Tanzania, Bi. Patricia Ngungulu (wa pili kushoto) na Muhasibu Mwandamizi Mwandamizi Mahakama ya Tanzania Bw. Venant Kambuga (wa kwanza kulia).(Picha na Innocent Kansha-Mahakama).

Jaji Mdemu alisema maeneo yote yatakayofundishwa na wawezeshaji ni muhimu na yanahusu utekelezaji wa majukumu yao kama Wahasibu na Wakaguzi wa Ndani kitaaluma na kimaadili. 

“Mtapewa nyenzo muhimu za utekelezaji kwenye maeneo mengine yaliyo nje ya taaluma yenu lakini hayaepukiki katika kuhakikisha mnatimiza wajibu wenu kutoa huduma ya kihasibu. Mlikuwa na mtakuwa na majadiliano mbalimbali ambayo yatawawezesha kubadilishana uzoefu katika kazi zenu, mkayatumie yote mtakayoyapata katika kufanyia kazi,”alisema Jaji Mdemu.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Mahakama 2020/2021-2024/2025 ambapo katika Tunu ya Tano kuhusu weledi, Mahakama itatekeleza majukumu ya utoaji haki kwa umahiri na ufanisi. 

Aidha, ndani ya Mpango Mkakati huo, katika nguzo ya kwanza inayohusu utawala, uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali, moja ya lengo ni kuwajengea uwezo watumishi wa ngazi zote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news