NA MWANDISHI WETU
WATU watano wamefariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya lori la mizigo lililobeba shehena ya mahindi kufeli breki na kugonga gari dogo la abiria aina ya Coaster lililokuwa likitoka Mbeya Mjini kwenda Wilaya ya Mbarali.

Amesema kuwa, lori la mizigo lililokuwa na tela liligonga gari la abiria na kisha kuliburuza mpaka kwenye vibanda vilivyopo pembezoni mwa barabara na kusababisha vifo hivyo na majeruhi.

Kamanda Matei amesema, miili ya watu waliofariki kwenye ajali hiyo imehifadhiwa kwenye kituo cha afya cha Inyala huku majeruhi wakipelekwa Hosptali ya Wilaya ya Igawilo ya Mbeya.