NA JUNIOR MWEMEZI-TARI
KAMANDA wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amesema Jeshi la Polisi linatambua mchango wa kilimo nchini na umuhimu wa utafiti katika kuendeleza kilimo kupitia Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) na wadau wengine katika mnyororo wa thamani.


Amesema, TARI iongeze nguvu katika kuwashauri wakulima ili kuongeza uelewa na kukifanya kilimo kuwa chenye tija.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), Dkt. Geoffrey Mkamilo ametoa hakikisho kuwa TARI itaendelea kusambaza teknolojia za kilimo kwa wananchi na kuwasaidia kulima kilimo chenye tija.
0 Comments