NAIBU WAZIRI MASANJA AKAGUA ENEO LILILOPANDWA MITI NA TFS MAGU

NA MWANDISHI WETU

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) Julai 20, 2022 amefanya ziara ya kushtukiza katika eneo la Shule ya Msingi Sagani lililopandwa miti kwenye Maadhimisho ya Siku ya Upandaji Miti Kitaifa yaliyofanyika Machi 21, 2022 Wilayani Magu Mkoani Mwanza.
Lengo la ziara hiyo ni kuangalia maendeleo ya miti iliyopandwa na Wakala wa Huduma wa Misitu Tanzania (TFS) endapo inatunzwa vizuri au la.

Mhe. Masanja amemuagiza Mkuu wa Shule ya Msingi Sagani, Ruhumbika Kapesa, kuendelea kusimamia ukuaji wa miti hiyo ili ifikie lengo lililokusudiwa la kuifanya Wilaya ya Magu kuwa ya kijani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news