Prof.Mkenda awapa taarifa njema Wanarombo kutoka kwa Rais Samia

NA MATHIAS CANAL

MBUNGE wa Jimbo la Rombo ambaye ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf Mkenda leo Julai 19, 2022 ameanza ziara ya kikazi ya siku saba jimboni kwake Rombo mkoani Kilimanjaro.
Katika ziara hiyo akiwa katika Kijiji cha Urauri Kata ya Reha, Prof.Mkenda ameeleza dhamira ya kuwatumikia wananchi katika jimbo lake na umuhimu wa kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama.

Amesema kuwa, kipindi cha nyuma kulikuwa na kampuni ya Kili Water ilioanzishwa kama kampuni ya kutoa huduma ya maji Rombo, lakini haikuwa na uwezo wa kutoa maji ya kutosha.
Amesema, wakati huo ilitolewa shilingi Bilioni nne pekee na Serikali kuimarisha upatikanaji wa maji jambo ambalo lililorudisha nyuma ulatikanaji maji hivyo kutofaa kwa mfumo huo ambapo kulipelekea kuiondoa kampuni hiyo ili kuimarisha upatikanaji wa maji.

Prof.Mkenda amesema kuwa katika hatua za kuimarisha upatikanaji wa maji serikali iliamua kuanzisha Bodi ya Maji Rombo inayoitwa ROMBOWASA ambayo inawajibika kutengewa bajeti na serikali kwa ajili ya sekta ya maji.

Mbunge huyo amesema kuwa kufuatia kuanzishwa kwa ROMBOWASA, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ametoa Bilioni 10 kwa wananchi wa Rombo kwa ajili ya upatikanaji wa maji ambapo hadi sasa wataalamu wanaangalia vyanzo vya maji ili kuhakikisha maji yanafika kwa wananchi.
"Rais Samia amekuja kuwatumikia watanzania na tayari kwa sasa ameonyesha njia na ninawahakikishia wananchi tatizo la maji litakamilika ndani ya muda mfupi.

"Rais Samia ameamua na amekusudia kuhakikisha maji yanapatikana na ndugu zangu wananchi nawahakikishia kuwa tuna Rais imara, mchapa kazi na hata waangusha wanachi wake kamwe,"amesema.
Prof.Mkenda amesema kuwa, katika ziara hiyo amekusudia kuwaeleza wananchi umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji na juhudi zinazofanywa na serikali kupitia Waziri wa Maji, Mhe.Juma Aweso za kumtua ndoo mama kichwani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news