NA DIRAMAKINI
WAZIRI wa Maliasili na Utalii Balozi, Dkt. Pindi Chana ametembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti na kupata maelezo juu ya kituo cha kutoa habari kidijitali (Serengeti Media Center) kinavyofanya kazi ya kutangaza vivutio, shughuli za hifadhi na za jamii zinazozunguka hifadhi hiyo.

Awali, Dkt. Chana alikutana na Menejimenti ya Hifadhi ya Taifa Serengeti ambapo Mkuu wa Hifadhi hiyo Kamishna wa Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Izumbe Msindai alitoa taarifa fupi kuhusu hifadhi.
