DED wa Temeke awatoa hofu wananchi juu ya mikopo asilimia 10

NA DIRAMAKINI

MKURUGENZI wa Manispaa ya Temeke mkoani Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya amewatoa hofu wananchi juu ya utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vijana,wanawake na watu wenye ulemavu.
Akijibu swali aliloulizwa na mmoja wa waandishi wa habari alipotembelea banda la Manispaa hiyo Agosti 4,2022 katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) mkoani Morogoro,Mkurugenzi Mabelya amesema kuwa, taratibu zote za utoaji wa mikopo hiyo hufuatwa.

"Nikuhakikishie kuwa utoaji wa mikopo upo wazi,hakuna kikundi chochote kinachopendelewa, utaratibu unaanzia kwenye kata husika , kikundi kinatakiwa kiandae andiko na kwa kifupi ni kwamba utoaji wa mikopo hii hufuata sheria na kanuni,"amesisitiza Mabelya.
Mabelya ametoa ufafanuzi huo wakati ambapo kumekuwa na taarifa nyingi za upotoshaji kuhusu utoaji wa mikopo hiyo kuwa inatolewa kwa upendeleo.

Awali akikagua baadhi ya shughuli zinazofanywa katika banda la Manispaa ya Temeke,mkurugenzi Mabelya alionesha kufurahishwa kwake mara baada ya kupata maelezo ya kina kutoka kwa wataalamu wa kilimo,mifugo na Uvuvi.
Moja ya matunda ya mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Manispaa ni wajasiriamali ambao wameshiriki katika Maonesho ya Nanenane mkoani hapa, ambapo wameweza kuleta bidhaa zao kuzitangaza na kuuza ili kujiongezea mapato.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news