MAMBO 10 YA RAIS SAMIA SULUHU KATIKA KUBORESHA MAZINGIRA YA SEKTA YA ELIMU

NA CHACHA WANGWE JR

TANGU alipoingia madarakani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan juhudi za kuboresha huduma kama vile Elimu, Afya na upatikanaji wa Maji safi na salama ni vipaumbele vilivyo wazi. Baadhi ya jitihada muhimu katika sekta ya Elimu;
1.Ujenzi wa Shule mpya za sekondari na shule ya msingi zipatazo 266.

2.Ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa ya shule za msingi, vituo shikizi, na shule za sekondari vipatavyo 18,219.

3.Ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi na sekondari vipatavyo 4,525.

4.Ukamilishaji ujenzi wa vyumba vya maabara vipatavyo 1,399.

5.Ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 568.

6.Ujenzi wa mabweni kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 170.

7.Ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari zipatazo 42.

8.Kutolewa ajira za walimu wapatao 9800 wa kada tofauti tofauti.

9.Watumishi katika wizara ya Elimu kwa maana ya walimu, waratibu wa Elimu na Maafisa Elimu kulipwa malimbikizo na madai yao yote yaliyohakikiwa.

10.Kutolewa fedha za Mikopo ya Elimu ya juu na kuondolewa kwa tozo ya VRF kiasi cha asilimia 6 kwa wanufaika wa Bodi ya Mikopo.

Rais Samia Suluhu anachapa kazi na anastahili pongezi za dhati kutoka kwa watanzania wote wenye mapenzi mema na nchi hii.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MMBARIKI RAIS WETU

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news