Mkurugenzi Mkuu wa TEA asisitiza jambo kwa watendaji wa halmashauri nchini

NA MWANDISHI WETU

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Bahati Geuzye amesisitiza umuhimu wa watendaji wa halmashauri nchini kushirikiana na TEA katika usimamizi wa miradi ya ujenzi wa miundombinu ya elimu inayofadhiliwa na Mfuko wa Elimu wa Taifa unaoratibiwa na TEA katika maeneo yao ili itekelezwe kwa ufanisi
Mkurugenzi Mkuu wa TEA alikuwa akitoa wasilisho katika Mkutano Mkuu wa 36 wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (ALAT) unaofanyika jijini Mbeya.

Amesema, katika mwaka wa fedha 2022/2023 kiasi cha Sh.bilioni 8.9 zimetengwa kwa ajili ya kufadhili miradi ya ujenzi wa miundombinu katika sehemu mbali mbali nchini
Miradi hiyo itahusisha ujenzi wa madarasa, matundu ya vyoo, nyumba za walimu na miudombinu ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news