Rais Samia atembelea eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa Msumbiji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea na kuweka shada la Maua katika eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa nchi ya Msumbiji (Mozambican Heroes’ Square) lililopo Maputo nchini humo tarehe 21 Septemba, 2022. Mhe. Rais Samia aliweka Shada hilo kwa Heshima ya kuwakumbuka Mashujaa wa Msumbiji akiwemo Rais wa Kwanza wa Nchi hiyo Hayati Samora Machel Viongozi mbalimbali kutoka Tanzania wakiwa katika eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa nchi ya Msumbiji (Mozambican Heroes’ Square) lililopo Maputo nchini humo tarehe 21 Septemba, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia vikundi vya ngoma za asili za Msumbiji wakati akitoka kuweka shada la maua kwenye eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa wa nchi hiyo (Mozambican Heroes’ Square) lililopo Maputo tarehe 21 Septemba, 2022. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Mji wa Maputo mara baada ya kutembelea Kituo cha uzalishaji wa Nishati ya Umeme nchini Msumbiji tarehe 21 Septemba, 2022.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news