Simiyu, Geita na Songwe wataja fursa lukuki za kiuchumi

NA DIRAMAKINI

LEO Septemba 24, 2022 viongozi wa mikoa ya Songwe, Geita na Simiyu wameshiriki mjadala wa Kitaifa juu ya maendeleo na fursa za kiuchumi zinazopatika katika mikoa hiyo.
Mjadala huo uliorushwa mubashara kupitia Mtandao wa Zoom na vyombo mbalimbali vya habari nchini umeandaliwa na Watch Tanzania huku viongozi hao wakitaja fursa mbalimbali na miradi inayotekelezwa na Serikali huko.

MHE.YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA WA SIMIYU

"Mkoa wa Simiyu ulipokea fedha nyingi zaidi kwa mwaka fedha 2021/2022 ulipokea karibia shilingi bilioni 29 kwa ajili ya utekelekezaji wa miradi ya maendeleo kwa upande wa barabara tulitengewa shilingi bilioni 14 na zilikuja shilingi bilioni 12, na kilomita 925 na madaraja 43 yalitengenezwa, 2022/ 2023 mkoa ulitengewa zaidi shilingi bilioni 11 kwa ajili ya miradi ya barabara.
"Tulipata fedha za miamala ya tozo zaidi ya shilingi bilioni 1.8 ambazo zilitengeneza zaidi ya kilomita 100 za barabara mpya ambazo zamani hatukuwa nazo.
"Kwenye Sekta ya Maji tuna mradi mkubwa Ziwa Victoria utakaotekelezwa kwa Wilaya ya Busega, Bariadi na Hitilima na vijiji 200 vitafaidika na mradi huu na awamu ya pili wilaya zitakazofaidika ni Meatu na Maswa,"amesema.

MHE.MARTIN REUBEN SHIGELA, MKUU WA MKOA WA GEITA

"Jambo zuri hapa Geita tuna Hospitali Rufaa ya Chato ambayo ni kubwa na kwa sasa imekua kama ya Kimataifa kwa sababu tunapokea wagonjwa kutoka baadhi ya nchi zinazotuzunguka kama Burundi, Rwanda na Uganda na kikubwa wanachokifuata ni huduma zetu bora.
"Kwa ujumla Awamu ya Sita chini ya Rais Samia kwa muda wake mfupi tangu aingie madarakani imeingiza zaidi ya Bilioni 600, ambazo zimelenga kuubadilisha Mkoa wa Geita, kiuchumi na miundombinu.
"Kuhusu mabadiliko ya tozo wengi wamefurahia kwa sababu wanaona mambo yanayofanyika, uzuri zaidi pesa zikija huwa zinaeleza kuwa ni pesa za tozo, na zinatumika kwenye miradi maalum na sisi kama mkoa tumejipanga vizuri sana kuhakikisha hii miradi iliyoanza kwa tozo inakamilika,"amesema.

MHE.WAZIRI WAZIRI KINDAMBA, MKUU WA MKOA WA SONGWE


"Songwe tuna usemi usemao ONGWE NI LAKO KUU LA SADC, kwa sababu majirani zetu wa nchi jirani wanatumia Mkoa wa Songwe kama njia ya kupitishia mizigo yao na sababu kubwa wenzetu hawana Bandari.

"Tunawakaribisha Watanzania kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Uvuvi, kwa sababu sisi hapa Songwe tunapakana na Ziwa Rukwa ambalo linatoa samaki wazuri na watamu, lakini pia kuna fursa ya ufugaji wa nyuki,"amesema.
"Kwenye eneo la utalii hapa Songwe tuna KIMONDO CHA MBOZI, kuna fursa ya kujenga hoteli na vivutio vingine, pia kwenye mkoa wetu tunawakaribisha wafanyabiashara kwa sababu Songwe ndiyo mkoa pekee uliokatikati ya nchi jirani.

"Sekta ya Afya hapa Songwe imepokea zaidi ya shilingi Bilioni 44 ambazo zimegawanywa kwenye maeneo mbaimbali ikiwemo Eneo la Mama na Watoto, Ununuzi wa Vifaa Tiba, Ujenzi wa Hospitali na Vituo vya Afya,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news