Yanga SC yaichakaza Zalan FC mabao 4-0

NA DIRAMAKINI

BAADA ya dakika 45 za awali kutamatika katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, hatua ya awali, Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam huku Zalan FC dhidi ya Yanga SC wakitoka bila bao.

Kipindi cha pili kimeanza kwa Yanga SC kupiga mpira wa nguvu ambao umewawezesha kuimiminia Zalan FC kutoka nchini Sudan mvua ya mabao.

Ikumbukwe kuwa, chini ya Kocha wa Yanga, Prof.Nasreddine Nabi alipokwenda mapumziko aliwapa mbinu mpya za kuibuka na ushindi.

Alianza Mayele dakika ya 47 kutupia bao ambalo liliwanyanyua mashabiki wa Yanga SC katika viti huku dakika ya 55 Feisal akitumbukiza bao la pili.

Mabao yaliyofuata ni ya Mayele ambapo hadi dakika tisini zinatamatika katika dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, Yanga SC imejizolea alama tatu ikiwa na mabao manne

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news