BRELA yashiriki maonesho yanayoendelea Pwani huku ikitoa wito kwa wadau

NA ROTARY HAULE

WAKALA ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) umewataka wadau mbalimbali wa biashara na wawekezaji kusajili jina la biashara au kampuni zao mapema kabla hawajaanza kufanya biashara.
Afisa Sheria wa BRELA, Aneth Mfinanga ametoa wito huo leo Oktoba 7, 2022 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya Tatu ya Uwekezaji na Biashara yanayofanyika katika viwanja vya stendi ya zamani Kibaha Mailimoja Mkoa wa Pwani.

Mfinanga amesema kuwa, moja ya changamoto wanayokumbananayo wakati wa usajili ni pale ambapo mtu anasajili jina la biashara wakati tayari lina mtu anayelitumia.

Amesema kuwa,wafanyabiashara wengi wanaanza kufanya biashara zao halafu baadae wanakwenda kusajili jina jambo ambalo limekuwa likileta changamoto katika usajili kwani wanapotaka kusajili wanakuta tayari analotaka kusajili lilishasajili muda mrefu.
"Nitumie nafasi hii kuwaomba wafanyabiashara wawe wepesi kusajili kwanza majina ya biashara na kampuni zao kabla ya kufanya chochote, kwa kuwa wengi wanaoenda kusajili wanakuwa tayari wameanza biashara na majina wanayotumia yanakuwa tayari yanatumika na watu wengine,"amesema Mfinanga.

Mfinanga amesema kuwa, endapo watakuwa wamesajili mapema itasaidia kuondoa usumbufu na kuwapunguzia adha ya kutafuta majina mengine hali ambayo itakuwa inawapotezea muda.

Amesema kuwa,BRELA imeshiriki Maonesho ya Wiki ya Biashara na Uwekezaji mkoani Pwani kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara kupata leseni zao,kusajili majina ya biashara na kampuni kirahisi.
Ameongeza kuwa,mteja anapofika kupata huduma hiyo wanapata cheti cha usajili papo kwa papo kwa kuwa teknolojia imekuwa na ni rahisi kuwahudumia wananchi.

Amesema,kila mkoa wamekuwa wakishiriki maonesho hayo na kwa upande wa Mkoa wa Pwani mwaka huu ni mara ya tatu kushiriki na wapo tayari huku akisema mhitiko wa wadau,wafanyabiashara na wawekezaji ni mkubwa bandani hapo.

"Kwa kweli tunashukuru maana mwitiko wa watu hapa bandani kwetu ni mkubwa,wapo wanakuja kutaka leseni,majina ya kampuni na hata majina ya biashara,"amesema Mfinanga.

Hata hivyo,amewataka wanachi,wadau, wawekezaji na wafanyabiashara kutembelea banda hilo la BRELA ili kupata huduma kwa wakati na kwamba watakuwepo katika maonesho hayo mpaka Oktoba 10, mwaka huu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news