Mhe.Gekul atoboa siri ya ushindi wa Serengeti Girls

NA SHAMIMU NYAKI

NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Pauline Gekul ameipongeza timu ya Taifa ya Wanawake chini ya Miaka 17 (Serengeti Girls) kwa ushindi wa magoli mawili kwa Moja dhidi ya Ufaransa.
Mechi hiyo ya Kundi D iliyochezwa Oktoba 15, 2022 Uwanja wa Pandit Jawaharlal Nehru jijini Goa, India imeipandisha Tanzania hadi nafasi ya pili nyuma ya Japan na mbele ya Canada na Ufaransa katika kundi hilo.
"Serikali ya Awamu ya Sita chini ya ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan inatoa mchango mkubwa kwa timu zinazowakilisha vyema nchi, na ndio maana hata nyie Serengeti Girls Serikali ipo hapa nanyi kuhakikisha inawaunga mkono mfanye vizuri," amesema Mhe. Gekul.

Kwa upande wake Kocha wa timu Bakari Shime, amesema vijana wanaendelea kuimarika na kusahihisha makosa ya Mechi ya kwanza dhidi ya Japan ambayo leo umeleta matokeo mazuri.
" Kesho tutaelekea Mumbai na tukifika tutafanya mazoezi kwa ajili ya mchezo na Canada ambao tukishinda tunasonga mbele," amesema Kocha Shime.
Tanzania ipo katika kundi D pamoja na Japan, Ufaransa na Canada.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news