VIJANA LINDI WADEKI BARABARA ILI KUMPOKEA RAIS SAMIA

NA DIRAMAKINI

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye ameungana na vijana wa Lindi kufanya usafi maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Lindi ikiwa ni maandalizi ya kumpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ambaye atawasili mkoani humo kesho Disemba 1, 2022.
Vijana hao walifanya zoezi hilo la kusafisha barabara baada ya kumaliza matembezi maalum katika maeneo mbalimbali ambapo walitumia fursa hiyo kufikisha salamu zao kwa Rais Samia kupitia kwa Waziri wa Habari, Mheshimiwa Nape.
"Sisi Vijana wa Lindi ilifikia hatua baadhi ya wanasiasa walituita watoto tuliotengwa, lakini walisahau licha Mkoa wa Lindi kutotembelewa na Rais kwa muda mrefu Mama yetu Samia Suluhu akiwa Makamu wa Rais alitutembelea sana,"amesema Mustafa Dumbo kwa niaba ya Vijana wa Lindi.
"Hivyo basi sisi vijana wa Lindi mbele ya Rais hatujihisi tuliotengwa kwa sababu alikua anatupenda kabla ya kuwa Rais wa nchi lakini hata sasa Mama Yetu ameendelea kuonesha upendi kwetu kwa kutupa vijana nafasi za ajira za Watendajinwa Kata, ametupa mikopo ya Halmashauri na Mikopo ya Bodaboda,"ameongeza Mustafa Dumbo.
Akiwajibu vijana Waziri Nape Nnauye amewataka vijana hao kutambua Rais Samia anawapenda sana mkoa wa Lindi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news