Watahiniwa milioni 1.07 wang'ara zaidi Matokeo ya Darasa la Saba 2022

NA DIRAMAKINI

WATAHINIWA zaidi ya milioni 1.07 kati ya milioni 1.34 wenye matokeo sawa na asilimia 79.62 wamefaulu kwa kupata madaraja A na B na C.
Kati ya hao wasichana ni 558,825 ambao ni sawa na asilimia 78.91 na wavulana ni 514,577 sawa na asilimia 80.41.

Hayo yamesemwa mbele ya waandishi wa habari na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), Athumani Amasi wakati akitangaza matokeo hayo leo Desemba Mosi, 2022 jijini Dar es Salaam.

Amasi alikuwa akizungumzia kuhusu matokeo ya mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika Oktoba 5 na 6,mwaka huu.

Pia amesema katika matokeo ya mwaka 2021 watahiniwa walikuwa 907,802 sawa na asilimia 81.97 ambapo kitakwimu kuna kupungua kwa ufaulu kwa asilimia 2.35 ingawa idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa watahiniwa 165, 600 sawa na asilimia 18.24 ikilinganishwa na mwaka 2021;

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

PSLE-2022 EXAMINATION RESULTS. Bonyeza jina la mkoa wako kuangalia matokeo ya shule uliyosoma au aliyosoma mwanao hapa chini;


ARUSHA

DAR ES SALAAM

DODOMA

IRINGA

KAGERA

KIGOMA

KILIMANJARO

LINDI

MARA

MBEYA

MOROGORO

MTWARA

MWANZA

PWANI

RUKWA

RUVUMA

SHINYANGA

SINGIDA

TABORA

TANGA

MANYARA

GEITA

KATAVI

NJOMBE

SIMIYU

SONGWE


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news