Rais Dkt.Samia awaapisha mawaziri, makatibu wakuu aliowateua

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (Mb) kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Februari, 2023.(Picha na Ikulu).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Balozi Mhe. Pindi Hazara Chana (Mb) kuwa Waziri wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 15 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Said Othman Yakub kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Februari, 2023.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (Mb), Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo (Mb) Balozi Mhe. Pindi Hazara Chana pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Said Othman Yakub wakila Kiapo cha Maadili kwa Viongozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, 15 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (Mb), Balozi Pindi Hazara Chana, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo (Mb) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Said Othman Yakub mara baada ya hafla ya Uapisho iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news