NA DIRAMAKINI
MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), zimekubaliana kushirikiana katika kuimarisha mapambano dhidi ya tatizo la dawa za kulevya na kupiga vita vitendo vya rushwa nchini.
Taasisi hizo zimefikia uamuzi huo baada ya kubaini kuwa, wafanyabiashara wa dawa za kulevya kwa kiasi kikubwa hutumia rushwa kufanikisha usafirishaji wa dawa za kulevya ambapo wamekuwa wakiwahonga watu wasiowaaminifu ili wawasaidie kukamilisha uhalifu huo katika maeneo mbalimbali nje na ndani ya nchi.
Ushirikiano huo utajikita zaidi katika utoaji wa elimu juu ya tatizo la dawa za kulevya na kupiga vita rushwa kwa wanafunzi kuanzia shule za msingi hadi vyuoni kupitia klabu za kupiga vita rushwa mbazo sasa zitatumika kupiga vita rushwa na dawa za kulevya.
Ameeleza kuwa,ushirikiano huo ni muhimu kwani utaisaidia sehemu kubwa ya jamii hasa wanafunzi ambao baadhi yao kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kulevya wakiwa katika umri mdogo, kufahamu madhara ya dawa za kulevya na hatimaye kutoshiriki kwenye matumizi na biasha ya dawa hizo.
Amehimiza kuwa, ni muhimu taasisi hizo zikajipanga kikamilifu katika kuhakikisha kuwa jukumu hilo linatekelezwa kwa ufanisi mkubwa.
Makubaliano hayo yamefanyika leo Aprili 14, 2023 jijini Dodoma, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAKUKURU yaliyohudhuriwa pia na baadhi ya Maafisa kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa.
Tags
Habari
Kataa Dawa za Kulevya na Timiza Ndoto Zako
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)
TAKUKURU Tanzania