Mama Mariam Mwinyi azindua Kliniki ya Aga Khan Zanzibar

NA DIRAMAKINI

MKE wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mariam Mwinyi amesema Shirika la Maaendeleo la Aga Khan (AKDN) limekuwa likijitahidi kuimarisha afya na ustawi wa jamii ulimwenguni kote pamoja na Zanzibar.
Mama Mariam Mwinyi ameyasema hayo leo Aprili 25, 2023 katika uzinduzi wa Kituo cha afya cha Kliniki cha Aga Khan jijini Zanzibar.
Ni kituo ambacho kitatoa huduma za dharura, huduma za kibingwa pia wagonjwa watapata huduma za afya zilizounganishwa kidijitali na Hospitali ya Aga Khan iliyopo jijini Dar es Salaam.
Amesema, Serikali ya Zanzibar inatambua umuhimu wa huduma bora za afya hivyo sekta hiyo imepata mageuzi makubwa ambayo yanajumuisha huduma za afya kwa ngazi ya shehia, wilaya hadi mkoa kupitia hospitali za rufaa ikiwa na jumla ya vituo vya afya 172 ambavyo vipo katika wilaya 11 Zanzibar.
Kwa upande wake Binti Mfalme Zahra Aga Khan amesema, uwekezaji kupitia Shirika la maendeleo la Aga Khan kupitia miundombinu ya huduma za afya ya Zanzibar inaonesha dhamira yake ya kuendelea kuboresha afya na ustawi wa jamii ulimwenguni kote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news