EWURA yatangaza bei za mafuta leo, Tazama bei hapa

NA DIRAMAKINI

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. 

Bei hizi zimeaanza kutumika kuanzia leo Jumatano, Mei 3, 2023 saa 6:01 usiku. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,Dkt.James A.Mwainyekule ambapo amesema kuwa,pamoja na kutambua bei hizo, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:-

(a) Kwa Aprili 2023, bei za rejareja za mafuta ya petroli na dizeli zilizopokelewa kupitia Bandari ya Dar es Salaam zimepanda kwa shilingi 90/Lita na shilingi 24/lita, mtawalia, ikilinganishwa na bei za toleo la tarehe 5 Aprili 2023.  

Pia,bei ya mafuta ya taa imepungua kwa shilingi 99/lita ikilinganishwa na bei ya toleo la tarehe 5 Aprili 2023.

(b) Kwa Mikoa ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara), bei za rejareja za Mei 2023 kwa mafuta ya petroli na dizeli zitaendelea kuwa zile zilizotangazwa katika toleo la tarehe 5 Aprili 2023kwa kuwa, kwa mwezi Aprili
2023, hakuna shehena ya Mafuta iliyopokelewa kupitia bandari ya Tanga.

Kwa mafuta ya taa, waendeshaji wa vituo kwenye mikoa ya Kaskazini wanashauriwa kuchukua mafuta hayo kutokea bandari ya Dar es Salaam.

Hivyo, bei za rejareja za mafuta ya taa katika mikoa hiyo italingana na gharama za kupokelea mafuta hayo kupitia Bandari ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.

(c) Kwa Mikoa ya Kusini (Mtwara, Lindi, and Ruvuma), bei za rejareja za Mei 2023 kwa mafuta ya petroli na dizeli zitaendelea kuwa zile zilizotangazwa katika toleo la tarehe 5 Aprili 2023 kwa kuwa, kwa mwezi Aprili 2023, hakuna
shehena ya Mafuta iliyopokelewa kupitia bandari ya Mtwara. 

Aidha, kwa kuwa hakuna matanki ya kuhifadhia mafuta ya taa katika bandari ya Mtwara,waendeshaji wa vituo vya mafuta kwenye mikoa ya kusini wanashauriwa kuchukua mafuta hayo kutoka katika bandari ya Dar es Salaam na hivyo bei za rejareja za mafuta ya taa katika mikoa hiyo itakuwa kulingana na gharama za kupokelea mafuta hayo kupitia Bandari ya Dar es Salaam na gharama za usafirishaji mpaka mikoa husika.

Bei za miji, wilaya na mikoa ni kama zinavyooneshwa katika Jedwali Na. 1. Aidha, tofauti ya bei kutoka sehemu moja kwenda nyingine inatokana na tofauti ya bandari mafuta yanapochukuliwa na gharama ya usafirishaji.

Mabadiliko haya ya bei yanachangiwa na kubadilika kwa bei za mafuta katika soko la dunia, gharama za usafirishaji (BPS Premium) na thamani ya shilingi ikilinganisha na dola ya Marekani.

Katika kutekeleza bei hizi, wafanyabiashara wa bidhaa za mafuta kwa jumla na rejareja pamoja na jamii kwa ujumla wanatakiwa kuzingatia yafuatayo: -

i. EWURA inapenda kuukumbusha umma kwamba bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli kwa eneo husika zinapatikana pia kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kisha kufuata maelekezo. Huduma hii ni bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya simu za mkononi hapa nchini.

ii. Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015, kifungu namba 166, beiza bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko. 

EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa za mafuta.

iii. Kampuni za mafuta ziko huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani mradi tu bei hizo zisivuke bei kikomo (Price cap) au kushuka chini ya bei iliyoruhusiwa (Floor Price) kama ilivyokokotolewa kwa mujibu wa Kanuni za EWURA za Kupanga Bei za Mafuta za Mwaka 2022 zilizotangazwa kupitia Gazeti la Serikali Na. 57 la tarehe 28 Januari 2022.

iv. Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana na yakionesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika. 

Pale ambapo inawezekana kuchagua, wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta katika vituo vinavyouza mafuta kwa bei nafuu zaidi ili kushamirisha ushindani. 

Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja. Adhabu kali itatolewa kwa kituo husika kwa kutotekeleza matakwa ya kisheria kwa mujibu wa kanuni husika.

v. Wauzaji wa mafuta ya petroli wanatakiwa kutoa risiti za mauzo kutoka kwenye mashine za EFPP (Electronic Fiscal Pump Printers) na Wanunuzi wahakikishe wanapata stakabadhi hizo za malipo zinazoonyesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita. 

Stakabadhi hizo za malipo zitatumika kama kidhibiti kwa wanunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya aidha kuuziwa mafuta kwa bei ya juu kuliko bei kikomo au kuuziwa mafuta yasiyo na kiwango cha ubora kinachofaa, na pia, risiti hizo zitasaidia kurahisisha ukusanyaji wa kodi za Serikali zitokanazo na mauzo ya mafuta ya petroli.

vi. Wafanyabiashara wa bidhaa za mafuta kwa rejareja wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei inayooneshwa katika Jedwali Na. 1. Hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mfanyabiashara yoyote atakayekiuka AGIZO hili.

vii. Wafanyabiashara wa bidhaa za mafuta kwa jumla wanatakiwa kuuza mafuta kwa bei inayooneshwa katika Jedwali Na. 2 isipokuwa kwa wateja wenye msamaha wa kodi. Hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mfanyabiashara yoyote atakayekiuka AGIZO hili.


JEDWALI 1: BEI KIKOMO ZA REJAREJA KWA SHILINGI/LITA
JEDWALI 2: BEI KIKOMO ZA JUMLA KWA SHILINGI/LITA

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news