Wamiminika katika Banda la OUT ndani ya Maonesho ya NACTVET Arusha

NA MWANDISHI WETU
Arusha

WAKAZI wa Jiji la Arusha wameendelea kumiminika kwa wingi katika banda la Maonesho la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) katika Maonesho ya Pili ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (TVET) ili kupata huduma na ushauri wa kujiunga na mafunzo ya elimu ya juu.
Maonesho hayo yanaratibiwa na Baraza la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) yanafanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kuanzia Mei 16 hadi Mei 22, 2023.
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinaendelea kuwakaribisha wageni wote kutembelea banda la chuo hiki lililopo uwanja wa Sheikh Amri Abeid kupata huduma mbalimbali ikiwemo maelezo ya kukifahamu zaidi chuo, kozi zinazotolewa, udahili, mifumo ya ufundishaji na ujifunzaji, utafiti, huduma kwa jamii na ushauri wa Kitaalamu.

Nyote Mnakaribishwa

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news