Wavutiwa na Huduma za Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) Maonesho ya NACTVET Arusha

NA MWANDISHI WETU

WANANCHI mbalimbali kutoka ndani na nje ya Jiji la Arusha wameendelea kumiminika katika banda la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) ndani ya Maonesho ya Pili ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (TVET) kupata huduma na ushauri wa kujiunga na mafunzo ya elimu ya juu.

Maonesho hayo yanaratibiwa na Baraza la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) yanafanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha kuanzia Mei 16 hadi Mei 22, 2023.

Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinaendelea kuwakaribisha wageni wote kutembelea banda la chuo hiki lililopo uwanja wa Sheikh Amri Abeid kupata huduma mbalimbali ikiwemo maelezo ya kukifahamu zaidi chuo, kozi zinazotolewa, udahili, mifumo ya ufundishaji na ujifunzaji, utafiti, huduma kwa jamii na ushauri wa Kitaalamu.

OUT ni nini?

Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) ni Chuo Kikuu cha Umma chenye mamlaka kamili, kinachojiendesha na chenye ithibati, kilichoanzishwa kwa Sheria ya Bunge Namba 17 ya 1992. 

Sheria hiyo ilianza kutumika Machi Mosi, 1993 kwa kuchapishwa kwa Tangazo la Serikali Na. 55 kwenye Gazeti rasmi la Serikali.

Kansela wa kwanza alisimikwa rasmi katika sherehe kamili Januari 19, 1994 na kundi la kwanza la wanafunzi lilidahiliwa Januari 1994. 
Mnamo Januari 2007, kufuatia kupitishwa kwa Sheria ya Vyuo Vikuu namba 7 ya 2005, OUT ilianza kutumia Mkataba na Kanuni za OUT (2007) kwa shughuli zake.

Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinatoa kozi zake za cheti, Stashahada, Shahada na Uzamili kupitia mfumo huria na masafa unaojumuisha njia mbalimbali za mawasiliano kama ana kwa ana,broadcasting, telecasting, correspondence, seminars, e-learning. Programu za kitaaluma za OUT zimehakikishwa ubora na zinadhibitiwa na Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).

Makao Makuu ya OUT yapo kwa muda nje ya Barabara ya Kawawa katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam. Makao makuu ya kudumu yanajengwa Bungo wilayani Kibaha, Barabara ya Soga, takribani kilomita 4.0 kutoka barabara kuu ya Morogoro mkoani Pwani.

OUT inafanya kazi kupitia mtandao wa Vituo vya Mikoa vipatavyo 30; Vituo 10 vya Uratibu, ambapo kimoja kiko Unguja na kimoja Pemba; viwili vipo Kenya (Egerton na Njoro), moja kipo Rwanda (Kibungo),Namibia na nyingine Uganda. 

Vituo vingine vya Uratibu wa Ndani vya OUT ni African Council for Distance Education -Technical Collaboration Committee (ACDE TCC),Centre for Economics and Community Economic Development (CECED) na SADC Centre of Specialization in Teacher Education (SADC ODL CoS TE). OUT pia ina Vituo 69 vya Utafiti vilivyoenea katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kinatoa vyeti vyake, Stashahada za kawaida, Shahada, Stashahada ya Uzamili na Uzamivu kupitia vitivo vyake vitano na taasisi mbili.

Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Jamii
Kitivo cha Usimamizi wa Biashara
Kitivo cha Elimu
Kitivo cha Sheria
Kitivo cha Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Mazingira
Taasisi ya Teknolojia ya Elimu na Usimamizi
Taasisi ya Elimu Endelevu

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news