AfDB yaonesha nia ujenzi reli ya kisasa

NA PETER HAULE-WFM 

BENKI ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na mambo mengine imeonesha nia ya kuongeza nguvu katika kusaidia utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa kwa Kiwango cha Kimataifa (SGR).
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa saba kushoto), Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya kibinadamu na kijamii, Bi. Beth Dunford (wa nane kulia), Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdalah Ulega (wa nane kulia), Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (wa sita kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Afrika, baada ya mkutano wao uliofanyika Ofisi za Hazina (Treasury Square) jijini Dodoma.(Picha na WFM).

Hayo yamebainishwa jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya Kibinadamu na Kijamii, Bi. Beth Dunford.

Amesema kuwa, AfDB imeonesha nia ya ushiriki kwenye mradi mkubwa wa kimkakati wa Reli ya Kisasa (SGR) kwenye baadhi ya maeneo ambayo hayajakamilika.
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt.Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (wa nne kushoto), ukiwa kwenye mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya Kibinadamu na Kijamii, Bi.Beth Dunford (hayupo pichani) jijini Dodoma.

Vilevile, benki hiyo imeonesha nia ya kushirikiana na Serikali kuongeza mtaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) ambayo ni chachu ya utekelezaji wa miradi ya kilimo kwa upande wa umwagiliaji na uongezaji wa thamani.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt.Mwigulu Lameck Nchemba (kushoto), akizungumza jambo wakati wa mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya Kibinadamu na Kijamii, Bi.Beth Dunford jijini Dodoma, mkutano huo umewashirikisha pia Waziri wa Kilimo, Mhe.Hussein Bashe (Mb) na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) pamoja na Makatibu wakuu na Manaibu Katibu Mkuu wa wizara hizo.

Amesema, maeneo mengine ambayo yamejadiliwa katika kikao hicho ni pamoja na miradi ya maeneo mahususi ya kilimo na kukuza ushiriki wa vijana katika shughuli za uzalishaji, mradi wa maeneo mahususi ya kilimo na mifugo.

Kuhusu wazo la Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan la kuanzishwa Benki ya Vijana, Dkt. Nchemba amesema kuwa, wamekubaliana timu ya wataalamu kukutana ili kuangalia namna jambo hilo linavyoweza kutekelezwa.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) akiteta jambo na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya kibinadamu na kijamii, Bi. Beth Dunford, nje ya jengo la Hazina (Treasury Square), baada ya kumalizika kwa mkutano ulioangazia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo ikiwemo maendeleo ya sekta Fedha, Kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Dkt. Nchemba ameishukuru Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kwa niaba ya Serikali ya Tanzania kwa msaada walioutoa katika sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo ya miundombinu, nishati, kilimo, maji na elimu.

Amesema kuwa, kiasi cha takribani dola za Marekani bilioni 2.6 kimetolewa na benki hiyo kwa ajili ya kutekeleza miradi 24, ambapo sekta ya kilimo imepewa asilimia nne ya fedha zote ambazo zimeletwa nchini kupitia Benki hiyo ambapo zinaboresha uzalishaji ikiwa ni pamoja na kukuza kilimo cha mazao kama ngano, alizeti na kuongeza kipato kwa mkulima.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdalah Ulega, akizungumza jambo wakati wa Mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya kibinadamu na Kijamii, Bi. Beth Dunford (hayupo pichani), jijini Dodoma, kulia ni Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb). 

Aidha, alieleza kuwa nchi za Afrika zilikubaliana kuongeza uwekezaji kwenye kilimo cha umwagiliaji, kuongeza thamani ya bidhaa na mazingira bora ya uhifadhi wa bidhaa jambo ambalo Serikali inalitekeleza kwa kuongeza bajeti kwenye sekta ya kilimo.

Alisema kuwa, Serikali imeongeza bajeti kutoka shilingi bilioni 294 kwa mwaka 2021/20222 hadi shilingi bilioni 970.8 kwa mwaka 2023/2024.
Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya kibinadamu na kijamii, Bi. Beth Dunford, akieleza kuhusu ushirikiano kati ya Benki hiyo na Serikali ambapo ameahidi Benki yake itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kuendeleza jamii jijini Dodoma.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya kibinadamu na kijamii, Bi. Beth Dunford, ameipongeza Serikali kwa juhudi zake za maendeleo na kuahidi kuwa AfDB itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kufanikisha miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya uzalishaji kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe, akieleza umuhimu wa maendeleo ya sekta ya kilimo, wakati wa Mkutano na Makamu wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika anayeshughulikia Sekta ya Kilimo na Maendeleo ya kibinadamu na kijamii, Bi. Beth Dunford (hayupo pichani), jijini Dodoma, kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdalah Ulega. 

Mkutano huo ulioongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Nchemba, umewashirikisha pia Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) pamoja na Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu wa Wizara hizo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news