Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa Kidato cha Tano na vyuo vya kati 2023

NA DIRAMAKINI

WANAFUNZI 188,128 waliokidhi vigezo wamechaguliwa na kupangiwa kujiunga na kidato cha tano katika shule mbalimbali nchini pamoja na vyuo vya fani mbalimbali.
Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2022 yanaonesha kuwa, watahiniwa 192,348 walipata ufaulu wa daraja la kwanza hadi la tatu ambapo kati yao Tanzania Bara walikuwa watahiniwa 188,128 wakiwemo wasichana 84,509 na wavulana 103,619.

Akizungumza na waandishi wa habari , leo Jumapili Juni 11, 2023 jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Angelah Kairuki amesema zoezi hilo limezingatia takwimu za matokeo ya wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2022 kutoka Tanzania Bara.

Amesema, wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka katika shule za serikali, binafsi, watahiniwa wa kujitegemea, waliofanya mtihani chini ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.

OFISI YA RAIS - TAMISEMI

UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2023


BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPANGWA KWENDA SHULE MOJA


CHAGUA MKOA ULIKOSOMA

ARUSHADAR ES SALAAMDODOMA
GEITAIRINGAKAGERA
KATAVIKIGOMAKILIMANJARO
LINDIMANYARAMARA
MBEYAMOROGOROMTWARA
MWANZANJOMBEPWANI
RUKWARUVUMASHINYANGA
SIMIYUSINGIDASONGWE
TABORATANGA

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news