TanTrade, Iran wakubaliana mema zaidi biashara na uwekezaji

NA MWANDISHI WETU

MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), Bi. Latifa M. Khamis amekutana na kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Balozi Hussein Alvandi Behineh, Balozi wa Jamhuri ya Kislamu ya Iran nchini Tanzania yaliyofanyika katika ofisi za Balozi.
Lengo la kikao hicho cha Juni 23, 2023 ni kujadili ukuzaji wa mahusiano ya kibiashara baina ya Tanzania na Iran Katika Biashara na Uwekezaji kwa Sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na afya, elimu na teknolojia.

Katika kikao hicho wamejadili kuhusu ushiriki wa Iran kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam ambapo kutakuwa na siku maalum ya Iran kwa ajili ya kuwakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania na Iran ili kubadilishana fursa baina yao.
Sambamba na hilo walijadili kuhusu kuratibu misafara ya kisekta zikiwemo afya, elimu na teknolojia mbalimbali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news