NA MWANDISHI WETU
WMJJWM, MBEYA
WAJANE nchini wameiomba Serikali kuwapatia msaada wa kisheria ili kupata haki zao na kusaidiwa huduma ya afya ya akili ili kudhibiti msongo wa mawazo.




Akijibu changamoto hizo, Waziri Mhe.Dkt.Gwajima amesema Serikali itaimarisha zaidi uratibu wa masuala ya wajane na kusimamia Sheria ya Msaada wa Kisheria Na. 1 ya mwaka 2017 kuhakikisha wajane wanapata haki zao.




