Watalaamu 132 wa HDU Hospitali ya Taifa Muhimbili wanolewa

NA MWANDISHI WETU

WATAALAMU 132 wamepatiwa vyeti vya kuhitimu mafunzo ya kuwasaidia wagonjwa wenye uhitaji mkubwa (Highly Dependent patients) yaliyotolewa na wauguzi bobezi wa wagonjwa mahututi (Critical care nurse specialist) na Madaktari bobezi wa mahututi.
Katika hatua nyingine madaktari na wauguzi 40 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ambao wanahudumia wagonjwa Mahututi wamepatiwa mafunzo ya kuboresha huduma katika maeneo ya kuzuia na kudhibiti maambukizi (IPC) , namna ya kutambua viashiria hatarishi na kuchukua hatua za haraka kwa kuwasaidia wagonjwa pamoja na kubadilisha mitazamo kwa watoa huduma.
Mafunzo hayo ya siku nne yaliendeshwa na wataalamu wawezeshaji kutoka Kitengo cha Ubora wa Huduma (Quality assuarance) Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ufadhili wa EMORY University na ABBOT Fund.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news