Mhandisi Kundo amaliza kazi Bunamhala

NA MATHIAS CANAL
Bariadi-Simiyu

WAKAZI wa Kijiji cha Giriku Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi mdogo wa udiwani unaotarajiwa kufanyika tarehe 13 Julai 2023 katika kata Bunamhala.
Uchaguzi huo utafanyika ili kukamilisha safu ya uongozi kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo marehemu Mheshimiwa Nhola Samora.

Akizungumza wakati wa mkutano wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi wa kata hiyo uliofanyika katika vijiji tofauti tofauti, Mbunge wa Jimbo la Bariadi mkoani Simiyu, Mhe. Mhandisi Kundo Mathew ameonya baadhi ya wanasiasa wanaowatishia wanachi watakaojitokeza kupiga kura.
"Hawa watu ni adui wa Maendeleo yoyote anayewaambia kesho msijitokeze kupiga kura ili kumchagua diwani wenu, huyo ni adui wa maendeleo,"amesisitiza Mhandisi Kundo.

"Anayezuia watu kumchagua kiongozi wao maana yake hataki maji, barabara, zahanati, umeme, kituo cha afya na dawa kwenye vituo cha afya." 
Mhandisi Kundo amesema kuwa, watu wanaofanya hivyo hawatakiwi kusikilizwa kwa namna yoyote kwani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema ataendelea kuboresha huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo upatikanaji wa dawa katika vituo vya afya.
Kuhusu changamoto ya upatikanaji wa maji katika kata hiyo Mheshimiwa Kundo amesema kuwa tayari serikali imesaini mkataba wa kuleta maji ya ziwa victoria hivyo wanachi wake mkao wa kula.

Katika uchaguzi wa nafasi ya diwani katika kata ya Bunamhala jumla ya vyama 14 vinatarajiwa kushiriki kinyang'anyiro cha nafasi hiyo katika uchaguzi utakaofanyika tarehe 13 Julai 2023.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news