Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete awapa somo wauguzi

NA LUSUNGU HELELA
Chalinze

NAIBU Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema taaluma ya uuguzi ni kazi ya uthubutu, utayari pamoja na kujitoa kwa ajili ya kuwahudumia wenye mahitaji ya kiafya huku akiwataka Wauguzi kuendelea kuchapa kazi kwa weledi na kwa kuzingatia miiko na maadili ya taaluma yao. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa na baadhi ya Viongozi na Wauguzi wakielekea katika Wodi ya Wazazi kwa ajili ya kuwajulia hali pamoja na kuwapatia zawadi mbalimbali kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.

Mhe. Kikwete ameyasema hayo Julai 22, 2023 wakati akizungumza na Wauguzi wa Mkoa wa Pwani kwenye Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze ambapo amewahimiza Wauguzi hao kuwahudumia wananchi kwa moyo na upendo wa hali ya juu. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa ameshika mshumaa na baadhi ya Wauguzi katika shamrashamara ya kuadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.

Amesema, Serikali inatambua kuwa Wauguzi ni kundi muhimu sana kwani ndio shina na mhimili mkubwa wa utendaji na ufanisi wa sekta ya afya nchini na ulimwenguni kote. 
Wauguzi wakiwa katika maandamano wakiadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani na kupokelewa maandamano hayo na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.

Mhe. Kikwete ametumia fursa hiyo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuweka mazingira mazuri ya kufanyia kazi Wauguzi hao ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati mbalimbali ili kuyafikia malengo endelevu ya afya kwa wote. 
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akikabidhi zawadi kwa Mariam Moyo aliyejifungua katika Wodi ya Wazazi iliyopo katika Hospitali ya Chalinze mkoani Pwani ikiwa ni shamrashamara ya Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza na Wauguzi wa Mkoa wa Pwani kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani ambapo amewahimiza Wauguzi hao kuwahudumia wananchi na jamii yote ya Kitanzania kwa moyo na upendo wa hali ya juu. 

Aidha, Mhe. Kikwete amesema Ofisi ya Rais-UTUMISHI inaendelea kuzifanyia kazi changamoto za kimuundo za taaluma hiyo na changamoto nyingine itaishirikisha Wizara husika ya Afya ili ziweze kufanyiwa kazi. 
Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Mganga Mkuu wa mkoa wa Pwani, Dkt. Gunini Kamba akizungumza na Wauguzi wa Mkoa wa Pwani kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kikwete amekubali ombi la kuwa mlezi wa Wauguzi katika Mkoa wa Pwani huku akiahidi kuwapa ushirikiano ili kuwaongezea morali Watumishi hao katika kutekeleza majukumu yao. 

‘’Natambua mchango wenu adhimu kwa mustakabali wa afya zetu kwani ziko mikononi mwenu, napenda kuwaahidi mimi kama mlezi wenu niko tayari kuwapa ushirikiano muda wote mtakaponihitaji,” amesisitiza Mhe.Kikwete. 
Sehemu ya Wauguzi wakimsikiliza Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete wakati akizungumza nao kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani ambapo amewahimiza Wauguzi hao kuwahudumia wananchi na jamii yote ya Kitanzania kwa moyo na upendo wa hali ya juu.

Awali Katibu wa Chama cha Wauguzi Mkoa wa Pwani, Bi, Dafroza Mnzava akisoma risala kwa Naibu Waziri Mhe. Kikwete, ameiomba Serikali kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili ikiwemo suala la muundo na posho ya mazingira hatarishi na stahiki mbalimbali. 

Pia Katibu huyo ameiomba Serikali kuendelea kuajiri wauguzi ili kuwawezesha kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wauguzi mara baada ya kukabidhi zawadi mbalimbali kwenye Wodi ya Wazazi katika Hosiptali ya Chalinze ikiwa ni katika kuadhimisha Siku ya Wauguzi Duniani iliyofanyika kimkoa katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoani Pwani.

Maadhimisho hayo yenye kauli mbiu “WAUGUZI WETU, MUSTAKABALI WA AFYA ZETU” yamefanyika mkoani humo ikiwa ni kuenzi kumbukumbu ya Muasisi wa Uuguzi na Ukunga Duniani, Bi. Florence Nightingale wa nchini Italia, aliyejitoa kwa moyo kuwahudumua wenye mahitaji ya kiafya. 

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news