Tudumishe mshikamano, fitina na majungu hapana-Dkt.Cherehani

NA MATHIAS CANAL

VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Ushetu wametakiwa kujenga ushirikiano na kuacha vitendo vya majungu na fitina ndani ya chama.
Pia,imeelezwa kuwa endapo kama watafanya mambo hayo yatawafanya wagawanyike katika makundi na kusababisha hata wanachama wa chama hicho wakose imani nao.

Aidha, wameelezwa kuwa CCM ni chama ambacho kipo madarakani kwa miaka mingi tokea nchi hii ipate uhuru, mikononi mwa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hivyo wanapaswa kuzingatia taratibu na sheria zilizowekwa kwa mujibu wa katiba husika ili wananchi wasiweze kujengeka na dhana potofu.
Mbunge wa Jimbo la Ushetu, Mheshimimiwa Dkt.Emmanuel Cherehani amesema hayo Agosti 4,2023 wakati alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Halmashauri ya Chama Cha Mapinduzi Kata ya Mapamba.
"Ndugu zangu hiki chama kilianza siku nyingi, viongozi hatupaswi kufanya majungu na fitina tufanye kazi kwa bidii kama tulivyoaminiwa na wananchi.”

Amesema kuwa, wanachotakiwa wakae na kujiuliza wametoka na wanakwenda wapi, huku wakiacha tabia za unafiki, uongo na fitina vitendo ambavyo kama wataviendekeza havitawafikisha mbali.
Amefafanua kuwa, Tanzania ni nchi ambayo wananchi wake wanapendana, hivyo chama kilichopo madarakani hakitakubali kuiacha rehani kwa watu wabovu ambao hawana nia njema na taifa.
Pamoja na mambo mengine aliongeza kuwa nchi haiendeshwi kwa mtindo kama wa kucheza bao, hivyo wameshauriwa kuwa makini na majukumu ya kazi zao za kila siku katika kutumikia wananchi.
Vilevile Mbunge Cherehani amegawa vifaa vya michezo ikiwemo mipira na jezi kwa ajili ya timu za mpira wa miguu katika vijiji vya Kata ya Mapamba kwa ajili ya kuimarisha sekta ya michezo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news